E FM

E FM
SIKILIZA 93.7 E FM KILA SIKU

Friday, May 30, 2014

VERY SAD: PICHA NA SAUTI MWANAFUNZI UDSM AFARIKI GHAFLA AKIWA AMEJIPUMZISHA CHUMBANI KWAKE...RAIS DARUSO ATHIBITISHA



TAARIFA za kusikitisha kutoka katika ofisi ya serikali ya wanafunzi ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ni kuwa mwanafunzi mmoja aliyetajwa kwa jina la Mwakimenya Sekabenga amefariki dunia ghafla mchana wa leo akiwa amepumzika chumbani kwake Hall 1 Block E .



Akizungumza na Suma the Presenter, Rais wa serikali ya wanafunzi ya Chuo hicho Bw. Filbert Nickson amethibitisha kutokea kwa kifo hicho na kusema kuwa, mpaka sasa hakuna taarifa rasmi hasa juu ya chanzo cha kifo hicho na kwamba tayari mwili wa marehemu umechukuliwa na kuhifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Taifa Muhimbili kwa ajili ya uchunguzi zaidi.



Rais ameeongeza kuwa mara baada ya taratibu za hospitali kukamilika, ofisi ya utawala wa chuo itahusika katika kusafirisha mwili wa marehemu nyumbani kwao Morogoro sambamba na ofisi ya serikali ya wanafunzi ya DARUSO.

 Rais wa DARUSO ametuma salamu za rambirambi kwa mwenyekiti wa UDBS, Bw. Frank  Mbwana, wanafunzi wa UDBS na UDSM kwa ujumla na kuwataka kuwa na subira katika kipindi hiki kigumu cha majonzi.

Mwakimenya Sekabenga alikuwa mwanafunzi  wa mwaka wa pili kutoka Shule ya Biashara (UDBS) akisomea shahada ya biashara ya Uhasibu.


Mungu ailaze roho ya marehemu pema peponi…. Aamen



No comments:

Post a Comment