“Nilipofika tuliishi vizuri, lakini 2012 alibadilika na kuanza
kuniadhibu, mara alinituhumu kutokufagia au kutopiga deki vizuri au
chakula kuwa na chumvi nyingi.
Mwanzoni alitumia fimbo alipohisi siumii alianza kuning’ata na kunichoma na pasi,” alisema.
Mwanzoni alitumia fimbo alipohisi siumii alianza kuning’ata na kunichoma na pasi,” alisema.
“Alinikataza kulia kwa sauti na kunitisha kuwa ataniua au kuniroga nikimwambia mtu yeyote yale aliyokuwa ananifanyia.”
Yusta anasema kuwa tajiri yake huyo alibadilika
zaidi baada ya kuondoka kwa mumewe ambaye hajui kama waliachana au
alihama kikazi.
“Mwaka 2012 mumewe aliondoka na hapo ndipo
matatizo yalizidi kwani hata mwanaye ambaye yuko kidato cha tatu
alimpeleka shule ya bweni hivyo tulibaki wawili tu na hakukuwa na mtu wa
kunisaidia,” anasema.
“Alinining’ata kila sehemu katika mwili wangu na
alipoona damu imejaa mdomoni alitema na kisha kuendelea kuning’ata mpaka
pale aliporidhika. Wakati mwingine alining’ata hadi usoni.”
Alisema alimfungia geti na kuondoka na funguo kila
alipotoka kwenda kazini na alipomtuma sokoni alimuamuru kwenda haraka
na kumkataza kuzungumza na mtu yoyote njiani hata majirani.
Aliongeza baada ya kuondoka kwa muwewe, Amina
alikuwa na kawaida ya kwenda kwa waganga wa kienyeji na wakati mwingine
waganga hao walifika nyumbani na kila walipofika alimfukuza na kumfungia
chumbani hivyo hakujua walikuwa wakifanya nini.
Alitokaje kwenye kifungo
Usiku wa Kuamkia Alhamisi ya Juni 5, binti huyo
alifanikiwa kutoka katika ‘kifungo’. Majirani wa Amina ambao walishidwa
kuendelea kuvumilia kusikia sauti za kilio cha Yusta mara kwa mara hasa
nyakati za usiku.
Majirani hao waliamua kupeleka taarifa za jambo
hilo kwa taasisi isiyo ya kiserikali ya Jipange ambayo inafanya shughuli
za kutetea wanawake. Baada ya kupata taarifa hizo, Jipange walitoa
taarifa polisi na hapo ndipo mtego wa kumnasa Amina uliwekwa na hatimaye
majira ya saa 8:00 usiku alikamatwa akiwa katika harakati za kukimbia
na kumtorosha Yusta ili kuficha ushahidi.
Mwenyekiti wa Jipange, Janet Mawinza alisema
walipopata taarifa za Yusta kutoka kwa wasamaria wema, waliwashirikisha
polisi, lakini kwa bahati mbaya taarifa zilivuja na kumfikia mtuhumiwa
hivyo alipanga njia ya kutoroka.
“Tulifika nyumbani kwa Amina majira ya usiku ili
kulinda mtu asitoke, lakini kumbe yeye alishafahamu ujio wetu, hivyo
aliruka dirisha na kukimbia. Alimkabidhi Yusta kwa kijana
aliyetayarishwa kumtorosha.”
Anaendelea kusema kwa bahati nzuri kwa kushirikiana na majirani
tulifanikiwa kuwazidi nguvu na hivyo mwendesha pikipiki aliyekuwa
akimtorosha Amina alikimbia na sisi kufanikiwa kumkamata. Hivyo
ilimlazimu na yule kijana aliyeondoka na Yusta kumpeleka kituo cha
polisi.”
Polisi wazungumzia
Mkaguzi msaidizi polisi wa Dawati la Jinsia, Mkoa
wa Kinondoni, Prisca Komba alisema suala la Yusta limefikishwa polisi
kituo cha Oystebay na mshitakiwa tayari amekamatwa na kufunguliwa jalada
namba OB/RB/9967/2014 kwa kosa la kujeruhi na upelelezi utakapokamilika
litapelekwa mahakamani kwa hatua zaidi. Kauli hiyo imeungwa mkono na
kaimu kamada wa polisi wa Mkoa wa Kinondoni, Thobias Edoyeka.
Alisema taarifa za binti huyo ziliwafikia baada ya
majirani kuzipeleka kwa kikundi kinachojulikana kwa jina la Jipange
kilichopo maeneo hayo ya Kwamanjunju na kikundi hicho kutoa taarifa
polisi na ndipo mtego wa kumnasa mwanake huyo ukawekwa.
Alisema majirani walikuwa wakisikia kelele za kilio mara kwa mara zikitokea ndani ya nyumba ya mtuhumiwa.
“Tumekagua makovu na majeraha mbalimbali yaliyo katika mwili wake na kupata jumla kuwa yako 91,” alisema Prisca.
”Tangu tumempata, amekuwa akinitaka nisiondoke
mbali naye kwa kuwa ana hofu. Lakini sasa afadhali kidogo baada ya
kumpatia ushauri na kumuhakikishia kwamba hapa yuko salama.”
Afisa wa Ustawi wa Jamii wa Mwananyamala, Rose
Temu naye alisema suala la Yusta liko mikononi mwao na wanafuatilia kwa
karibu matibabu pamoja na usalama wake.
Akutana na mama yake
Siku ya Jumapili Juni 8 Mwananchi ilimtembelea
Yusta kwa mara ya pili. Ilikuwa ni muda wa kuona wagonjwa saa 6:00
mchana kumbe miongoni mwa watu waliohitaji kumuona, alikuwepo na mama
yake mzazi aitwaye Modesta Simon.
Ilikuwa ndio mara ya kwanza kwa wawili hao
kukutana baada ya miaka mitatu ya mateso. Modesta alifika jijini
akitokea Tabora kwa lengo la kumwona binti yake baada ya kusikia taarifa
zake kupitia vyombo vya habari na ndugu yake aliyeko Arusha.
Ulikuwa ni wakati wa furaha na huzuni. Ulikuwa
wakati mgumu kwa mama huyo kuamini hali aliyomkuta nayo mwanae. Vilio
vilitawala hali iliyowafanya ndugu wa baadhi ya wagonjwa waliolazwa
katika wodi hiyo kujaa katika kitanda cha Yusta.
Mara baada ya mama huyo kuingia wodini, Yusta aliyekuwa ameketi
kitandani aliruka na kumkimbilia mlangoni na kilichofuata ilikuwa vilio.
Akizungumza huku akimkagua mwilini na kutokwa na
machozi, Modesta alisema: “Jamani, Amina kweli amekufanya hivi. Kila
nikiuliza wananiambia hujambo kumbe umeharibika hivi?
“Amina ni mtoto wa mjomba wangu kabisa na sikuwahi
kuambiwa chochote, niliamini mnaishi vizuri. Sikudhani kama anaweza
kulifanya jambo hili.”
Modesta alisema awali alikuwa na mawasiliano na
mwanae kwa kutumia simu ya mama yake Amina ambaye wanaishi karibu,
lakini hivi karibuni alianza kupata wasiwasi baada ya kila alipohitaji
kuongea naye, alipewa sababu hivyo akaomba Yusta kurudishwa na
aliahidiwa angepelekewa mwezi huu.
“Alinihahidi mwezi huu angemleta Yusta nyumbani.
Alisema anataka amnunulie cherehani ili akija apate shughuli ya
kufanya,” alisema.
Alisema anaviachia vyombo vya sheria katika
kumpatia haki binti yake na anatamani kuona Amina anaadhibiwa kulingana
na kosa alilolitenda.
Kwa upande wake, Yusta alisema amefurahi kukutana na mama yake kwani sasa ataweza kumweleza mateso yake yote kiundani.
“Nimefurahi polisi waliponiambia mama anakuja,
sasa nina furaha zaidi nimemuona... nitaweza kuongea naye. Sikuweza
kumueleza kwenye simu kwa sababu Amina alikuwa akinisimamia kila
aliponipa simu niongee naye,” alisema.
“Madakatari wameniambia nimeruhusiwa. Mama akiondoka nataka twende wote, sitaki tena kubaki hapa”
Yusta alisema akipata pesa za mtaji angependa
kujishughulisha na utengenezaji batiki na pia ushonaji, kwani hizo ndizo
fani anazozipendelea zaidi katika maisha yake.
Afisa muuguzi katika wodi aliyolazwa Yusta, Erica
Massawe alisema hali ya binti huyo imeimarika na tayari alisharuhusiwa
kutoka tangu Juni 6, hivyo wanasubiri maelekezo ya polisi na Ustawi wa
Jamii ambao ni wahusika wakuu katika shauri la binti huyo.
“Tunasubiri polisi ili tuwapatie hati ya ruhusa
(discharge) na PF 3 kwani haturuhusiwi kumkabidhi kwa ndugu, hata
akitembelewa anakuwa chini ya uangalizi wetu,” alisema.
Usuli
Yusta alitoka hospitali Jumatatu ya Juni 9 na
kukabidhiwa kwa kikundi cha wanahakarati wa kutetea haki za wanawake
(Jipange) baada ya majadiliano baina ya mama yake, kamati ya ulinzi na
usalama kata ya makumbusho na ofisa mtendaji kata ya makumbusho.hii mi
kwa ajili ya kurahisisha binti huyo kufika mahakamani pindi
atakapohitajika kufanya hivyo.
Chanzo: GAZETI LA MWANANCHI
No comments:
Post a Comment