E FM

E FM
SIKILIZA 93.7 E FM KILA SIKU

Monday, May 11, 2015

BRAND NEW TRACK: D-MALICK - 'NIPE KIDOGO'. ISIKILIZE NA UIDOWNLOAD HAPA

KAMA ulipata time ukasikiliza Bongo Fleva ya Clouds FM Jumamosi iliyopita, basi jina D-MALICK haliwezi kuwa geni saaana.. Ila pia kama hukusikiliza basi Suma255 inakuletea msanii mpya kabisa
kwenye game ya Bongo Fleva anayeitwa Abdulmalick Simbamgeni ambaye kisanii anajulikana kama D-MALICK. 

Jamaa kashare na sisi birthday yake ambayo ni tarehe 03/03/1990 ambaye kwa sasa ni mwanachuo wa Chuo cha The Institute of Social Work akisomea shahada ya kwanza ya 'Industrial Relations'. D- MALICK kaja kwako mtanzania kwa mara ya kwanza kaachia wimbo unaoitwa 'NIPE KIDOGO' ambao umeandaliwa chini ya studio za BMK/FIDECASTRO MUSIC. 

Hili ni bonge moja la ngoma of course cha kufanya ni kuidownload na kuirequest kwenye vituo mbali mbali vya redio nchini. Unaweza kuwa karibu na D-MALICK kwa kumcheki Instagram na Twitter kupitia @dmalickdreams na Facebook @ D Malick Mnyamwezi

Unaweza kudownload 'Nipe Kidogo' ya D- Malick Hapa

No comments:

Post a Comment