E FM

E FM
SIKILIZA 93.7 E FM KILA SIKU

Sunday, June 15, 2014

RONALDO BADO HALI MBAYA...INAWEZEKANA ASICHEZE MECHI DHIDI YA UJERUMANI


CRISTIANO RONALDO amezua tena wasiwasi kwa mashabiki wa Ureno baada ya jana asubuhi kuonekana akitoka katika hoteli akiwa na barafu katika goti lake la kushoto huku wakijiandaa na mchezo mgumu wa kwanza dhidi ya Ujerumani.
Nyota huyo wa Real Madrid ni tegemeo katika kikosi cha Ureno, lakini Ronaldo mwenye miaka 29 anaweza kuwakosesha raha mashabiki kama maumivu aliyoyapata tangu akiwa katika klabu yake yanaendelea.

Ronaldo alifanikiwa kufanya mazoezi na wachezaji wenzake kwa dakika 20 kabla ya kulazimika kutoka.

Ronaldo alionekana kusaini fulana za mashabiki kabla ya kukaa kwenye benchi akiwaacha wenzake wakiendelea.
 
Mshindi huyo wa tuzo ya ubora wa dunia ya ‘Ballon d’Or 2014’ alishapumzika kwa wiki mbili kutokana na maumivu ya goti kabla ya fainali za Kombe la Dunia.

Kurudi kwa matatizo hayo kunaweza kuwa matatizo makubwa kwa kikosi cha Ureno chini ya kocha Paulo Bento, ambao wanamtegemea nahodha huyo.

Inatarajiwa kuwa, Ronaldo, ambaye hata hivyo haonekani kama anajisikia maumivu, ataanza katika mchezo wa kwanza kwa Ureno katika fainali za Kombe la Dunia, lakini kujulikana kwa uzima wake halisi bado tatizo.

No comments:

Post a Comment